
BODI ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imesitisha kwa muda mikopo kwa wanafunzi 2,739 walioshindwa kujitokeza wakati wa kuhakiki wanufaika wa mikopo hiyo.
Aidha, imetoa siku saba kuanzia jana kwa wanafunzi ambao hawakuhakikiwa kwenda kuhakiki katika vyuo vyao, vinginevyo mikopo yao itafutwa na kutakiwa kurejesha kiasi walichokopeshwa na kuchukuliwa hatua za kinidhamu.
Akizungumza...