KINGAZI BLOG: 05/15/16

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Sunday, May 15, 2016

Vijana Wanaovaa Suruali Chini ya Kiuno Kuchapwa Viboko 70

Wakazi wa Kata ya Karansi, Wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro wametoa uamuzi kuwa wanawake watakaovaa sketi fupi na vijana watakaovalia suruali chini ya kiuno, wataadhibiwa kwa kuchapwa viboko 60 hadi 70.   Uamuzi huo umefikiwa na wakazi zaidi ya 200 wakisema uvaaji huo ni kinyume na mila na desturi za Kiafrika.   Vazi lingine lisilotakiwa kwa wanawake ni kuvaa suruali pamoja na vijana...

Machangudoa waitaka serikali itambue biashara yao. Na walipe kodi pia.

Baadhi ya wanawake wanaojiuza katika mitaa ya Majengo B na Fisi, mjini Mpanda mkoani Katavi wameitaka Serikali kuandaa utaratibu wa kuwatambua ili nao waweze kulipa kodi na kuliingizia taifa pato kutokana na shughuli wanayofanya ya kuuza miili yao. Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana usiku, baadhi yawanawake hao walisema wanafanya kazi kama zilivyo kazi nyingine kwani zinawaingizia kipato kizuri...

Serikali Yanasa Kilo 34,000,000 za Sukari iliyofichwa.

Shehena ya sukari ya kilo milioni 34 zilizokuwa zimefichwa kwenye maghala ya wafanyabiashara watatu Kilimanjaro imekamatwa na vyombo vya usalama, na serikali mkoani humo imetangaza kuiuza kwa wananchi kuanzia jana kwa bei elekezi ya Sh. 1,800. Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Said Mecki Sadiki alithibitisha jana kukamatwa kwa shehena hiyo, baada ya makachero wanaoongoza timu maalumu ya ukaguzi wa maghala...

Rushwa inahitaji nguvu ya pamoja kuikomesha-Majaliwa

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema mkutano wa kimataifa uliojadili jinsi ya kupambana na rushwa duniani ni kiashiria kwamba tatizo la rushwa ni kubwa sana na linataka juhudi za pamoja kukabiliana nalo. Alitoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki wakati akizungumza na Waziri wa Nchi wa Uingereza anayeshughulikia Maendeleo ya Kimataifa, Justine Greening walipokutana kwenye mkutano huo uliofanyika...

WHO yaeleza kuwa hewa chafu yazidi kuathiri dunia

Utafiti huo umegundua kwamba hali chafu ya hewa imeongezeka mara mbili zaidi ikilinganishwa na miaka miwili iliyopita katika miji elfu 3 kwenye nchi 10...

DC Kinondoni akemea vigogo wa sukari wanaompigia simu

MKUU wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi amefichua kuwa amekuwa akipigiwa simu na baadhi ya wafanyabiashara vigogo wenye nia ya kutaka kupunguza makali ya operesheni inayofanywa na wilaya yake dhidi ya waficha sukari. Kwamba simu hizo amekuwa akipigiwa hadi usiku wa manane na huku wengine wakimtumia ujumbe mfupi wa simu wa maandishi (SMS). Amekemea wafanyabiashara hao na kutaka waache mara moja mchezo...

Magazeti ya Tanzania yalichoandika leo jumapili Mei 15 kwenye habari za kitaifa,kimataifa na michezo.

Mei 15naanza kwa kukuletea habari zilizoandikwa kwenye magazeti ya Leo kwenye habari za kitaifa kimataifa na michezo ili ujue kilichojiri duniani.Pia usiache kukaa karibu nasi kwenye mitandao ya kijamii yaani Facebook@tanzaniampyasasa blog ma Twitter @Tanzaniampyasasa.karibu. ...

Mashine "iliyotumbuliwa" na JPM Uwanja wa Ndege Imepona na Inafanya kazi Kwa Ufasaha

Hatimaye mashine iliyotembelewa na Rais JPM jana na kukutwa ikiwa mbovu au haifanyi kazi kwa ufanisi sasa inapiga mzigo kama kawaida na ikiwa chini ya uangalizi wa Maafisa Usalama wa Mamalaka ya Viwanja vya Ndege,Polisi na Afisa wa TRA. Mashine hiyo aina ya Rapscan inayotumika kukaguwa mizigo ya abiria wanaoingia Dsm kutoka Znz,na mikoa mingine ya Tanzania,mapori ya Utalii kama Selous,Mikumi,Sadani...

UN: Uhusiano wa Boko Haram na IS ni tishio

BOKO HARAM Uhusiano wa Boko Haram na Islamic State Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa limeelezea wasiwasi wake kuhusu kasi ya kuimarika kwa ushirikiano kati ya kundi la wapiganaji la Boko Haram nchini Nigeria na lile la Islamic State, wakati Nigeria inaandaa kongamano la kupambana na kundi hilo la kigaidi. Katika taarifa kwa vyombo vya habari, baraza hilo la wanachama 15 limesema kuwa Boko Haram...

JINSI TABIA INAVYOWEZA KUKUFANIKISHA AU KUKUFELISHA MAISHANI

Michael Jackson. Kama vile mmea unavyoweza kupandwa kwenye mbolea ukaota, kukua na baadaye kuzongwa na magugu ambayo huudumaza na hatimaye kama hayatang’olewa kuua, ndivyo ndoto za mwanadamu na mafanikio yanayoweza kujengewa tabia njema ya kukua lakini baadaye tabia mbaya ambazo huja na mafanikio zikaua kila kitu. Withney Houston. Ili mwanadamu afanikiwe maishani mwake ni lazima awe na tabia pamoja...

Waziri Mkuu: Tanzania Kushirikiana Na Jumuiya Ya Madola

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Jumuiya ya Madola inaweza kuiga mbinu ambazo Tanzania imetumia katika kupambana na rushwa zikiwemo za kujumuisha wadau tofauti kwenye vita hiyo. Ametoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki wakati akizungumza na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola, Bibi Patricia Scotland walipokutana kwenye mkutano wa kimataifa uliojadili jinsi ya kupambana na rushwa duniani uliofanyika...

Chelsea yawapa tuzo wachezaji wake, Terry abaki

Matajiri wa London timu ya soka ya Chelsea jana usiku ilifanya hafla fupi yakuwatuza wachezaji wake waliofanya vema katika michuano mbalimbali kwa msimu huu wa 2015/2016. Katika tuzo hizo nyota wa Brazil, Willian amefanikiwa kufunika usiku huo baada ya kutwaa tuzo mbili kubwa moja ya kuwa mchezaji bora wa mwaka wa labu hiyo na nyingine ya kuwa mchezaji Bora Chaguo la Wachezaji wa Mwaka wa klabu...
 

Gallery

Popular Posts

About Us