KINGAZI BLOG: 08/03/16

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Wednesday, August 03, 2016

Arsernal kutwaa taji chini ya Arsene Wenger ni ndoto_ Sutton

Mshambuliaji wa zamani wa Chelsea na Celtic Chris Sutton amepigilia msumari wa moto kwa Arsenal kwa kusema kwamba kamwe wasitarajie ubingwa kama timu hiyo itaendelea kuwa chini ya Arsene Wenger.

Katika dirisha hili la usajili Arsenal wamemsajili Granit Xhaka tu, huku wenzao Manchester City, Manchester United na Chelsea wakiwa wamefanya usajili wa maana kuimarisha vikosi vyao kwaajili ya msimu mpya.

Sutton ambaye alibeba kombe la Ligi ya England akiwa na Blackburn Rovers, amemlaumu Arsene Wenger kwa kutoonesha nia ya dhati ya kufanya usajili wa kusiaidia timu na kusisitiza Mfaransa huyo anahitaji kuachia ngazi kwa manufaa ya timu.

“Nina mashaka makubwa na Arsenal katika msimu huu tena. Hawajaonesha nia yoyote mpaka sasa,”Sutton aliiambia BBC Five Live.

“Nadhani bodi na Wenger wanawaangusha sana mashabiki wao. Mimi sijui ni wapi Arsenal wanaelekea, kama ningekuwa ni shabiki wa Arsenal, basi ningehuzunika sana.

“Wamesema hatawatumia fedha nyingi, bodi inafurahia tu jambo hili, au uongo? Kila mwaka, wao kazi yao ni kushiriki Ligi ya Mabingwa na kupata fedha.

“Wenger sio kocha mwenye malengo na Arsenal tena, alikuwa na nafasi kubwa ya kushinda taji msimu uliopita, lakini alishindwa. Hawataki kutumia pesa, na kama wewe ni shabiki wa Arsenal, jitathmini vizuri, maana kila mwaka itakuwa ni mwendo wa ‘top four’ tu.

Halafu unaona timu kama Manchester United, Manchester City wanaonesha nia ya ubingwa msimu huu, hili linazidi kuleta ugumu zaidi kwa Arsenal, nasema hivi….mpaka Wenger aondoke ndipo Arsenal watatwaa ubingwa.”

PICHA ZA UTUPU ZA MKE WA TRUMP ZAVUJA

IMEVUJAA hatimaye picha za uchi za mke wa mgombea urais wa Marekani kwa tiketi ya Chama cha Republican, Donald Trump aitwaye Melania Trump zimevujaa na kusambaa kwa kasi kwenye mitandao mingi ya kijamii.

Picha hizo zilipigwa tangu mwaka 1995 miaka mitatu kabla ya kukutana na Trump, wakati huo Melania akiwa na umri wa miaka 25 na kuchapishwa kwa mara ya kwanza kwenye gazeti la New York Post mwishoni mwa wiki iliyopita na kurudiwa tena kwenye gazeti la jana Jumatatu.

Picha za utupu za mke wa Trump zilizovuja mitandaoni.

Gazeti lililotoa picha hizo.

NDEGE YA EMIRATES YAWAKA MOTO IKIWA NA WATU 300


Ndege ya Shirika la  Emirates iliyokuwa ikijiandaa kutua katika Uwanja wa Kimataifa wa Dubai imewaka moto  na kusababisha taharuki kubwa kwa abiria waliokuwamo kwenye ndege hiyo.

Ndege hiyo Boeing 777 ilikuwa na abiria 282 na wafanyakazi 18 na hakuna aliyejeruhiwa. Abiria wote waliokolewa kupitia mlango wa dharura wa ndege hiyo iliyouwa ikiruka kutoka Trivvandrum, India.

Waliondolewa kwenye eneo la tukio ndani ya dakika 45 tangu kwa ndege hiyo kuwaka moto huku vyombo vya zimamoto zikichukua hatua ya haraka kuudhibiti moto huo.

Ndege hiyo iliwaka moto muda mfupi baada ya kutua kwenye uwanja huo na kwamba hadi sasa hakuna taarifa za kile kilichobabisha kuzuka kwa moto huo.

Basi linalotembea majini na nchi kavu lazinduliwa China

 Amini usiamini hili ni basi la kipekee linaloruhusu magari kupitia chini yake

Basi la kipekee lenye urefu wa mita mbili juu linaloruhusu magari ya kibinafsi kupitia mvunguni mwake limefanyiwa majaribio katika mji waHebei kaskazini mwa Uchina.

Basi hilo linalopigiwa upatu kutatua kabisa tatizo la usafirishaji wa watu katika miji yenye idadi kubwa ya watu ama Transit Elevated Bus (TEB) limefanyiwa majaribio nchini China.

Basi hilo linaloendeshwa kwa umeme linauwezo wa kubeba zaidi ya watu 300 .

Basi hilo kubwa lina urefu wa mita 21 na upana wa futi 25 .

Hii ndio mara ya kwanza kwa wabunifu kuonesha basi hilo hadharani baada ya video yake kuvuja katika mitandao mwezi Mei.

 Ndani inanafasi kubwa mno inaweza hata kuwabeba abiria 300

 Basi moja la TEB linauwezo wa kubeba abiria wote katika mabasi 8 ya kawaida !

Majaribio ya basi hilo la kipekee yalifanyiwa katika barabara iliyofanyiwa ukarabati yenye urefu wa mita 300m.

Basi hilo linauwezo wa kuhudumu kwa kasi ya Kilomita 60 kwa kila saa.

Takriban mabasi hayo manne yanawezwa kuunganishwa na hivyo kuwa na dereva mmoja.

Hivi ndivyo inavyoonekana

''Mabasi haya ni ya kipekee na moja ya faida yake kuu ni uwezo wake wa kubeba abiria wengi sana 300 kwa kila basi, pia itaokoa sana nafasi barabarani'' alisema mhandisi mkuu katika mradi huo mpya wa usafiri Song Youzhou.

''Inahudumu kama vile treni za kisasa za umeme ila gharama ya kuwekeza kujenga njia na ukarabati barabarani ikiwemo ujenzi wa vituo maalum vya TEB ni 1/5 ''

VYUO 175 NCHINI VYAPEWA NOTISI YA KUSHUSHWA HADHI NA NACTE

Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE), Mhandisi Steven Mlote(kushoto)akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam,wakati wa kutoa tamko la baraza hilo kuvifutia Usajili baadhi ya vyuo na vyuo 175 vimepewa notisi ya kushushwa hadhi,5 vyafutiwa Usajili na 41 vimetakiwa kujisajili mara moja,ikiwa katika jitihada za kuboresha elimu ya ufundi nchini,ikiwa katika jitihada za kuboresha elimu ya ufundi nchini,Katikati Kaimu wa baraza hilo Dkt. Adolf Rutayuga na Mkurugenzi wa Udhibiti,Ufuatiliaji na Tathimini Bi. Agness Ponera

Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) limetangaza kuwa vyuo 5 vimefungwa kuendesha mafunzo na kufutwa kwenye rejista ya vyuo vya ufundi nchini.

Pia Baraza limetangaza kuwa vyuo 41 vinavyotoa elimu ya ufundi bila kusajiliwa kwa mujibu wa sheria vimepewa muda wa wiki mbili na kutakiwa vijisajili mara moja kwenye Baraza hilo kabla ya kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

Vilevile, vibali vya usajili wa vyuo 112 vya kutoa elimu ya ufundi vimefikia ukomo hivyo vinapaswa kutekeleza masharti ya Usajili; wakati vyuo 57 vimefikia ukomo wa ithibati, hivyo inapaswa kutekeleza masharti ya ithibati, imetangazwa jana.

Akiongea katika mkutano na waandishi wa habari, Mwenyekiti wa Baraza (NACTE), Mhandisi Steven Mlote, amesema Baraza limetoa muda wa mwezi mmoja kwa vyuo 112 kutekeleza masharti ya usajili na vyuo 52 kutekeleza masharti ya ithibati kwa mujibu wa sheria za uendeshaji vyuo vya ufundi nchini, na vyuo vitakavyoshindwa kutekeleza agizo hili vitafungiwa mara moja.

Mhandisi Mlote pia alitoa onyo akisema “vyuo 41 vinavyotoa elimu ya ufundi bila kusajiliwa kwa mujibu wa sheria nimevipa muda wa wiki mbili na navitaka vijisajili mara moja kwenye Baraza kabla ya kuchukuliwa hatua kali za kisheria”.

Mhandisi Mlote alivitaja vyuo vyote vyenye matatizo kama ifuatavyo:












 

Gallery

Popular Posts

About Us