
NAIBU Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Yussuf Masauni amesema askari wa usalama barabarani watakaobainika kupokea rushwa watashughulikiwa kwa kuwa wataweka mitego kwa ajili ya kuwakamata.
Alisema wananchi wamekuwa wakilalamikia askari hao kuwa wanapenda rushwa na ndio chanzo cha ajali barabarani na kwamba wanachafua taswira ya jeshi hilo.
Akizungumza na askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani,...