KINGAZI BLOG: Chadi

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...
Showing posts with label Chadi. Show all posts
Showing posts with label Chadi. Show all posts

Monday, May 30, 2016

Habre ahukumiwa kifungo cha maisha jela.


Image copyrightAFP
Image captionHabre alipatikana na makosa ya uhalifu dhidi ya ubinadamu , ubakaji na utumwa wa ngono.
Aliyekuwa rais wa Chad Hissene Habre amehukumiwa kifungo cha maisha jela baada ya kupatikana na hatia ya kuhusika kwenye uhalifu dhidi ya ubinadamu , ubakaji na utumwa wa ngono.
Hissene Habre alihusika moja kwa moja katika uhalifu huo ambao ulifanyika wakati akiwa rais wa Chad.
Waathiriwa waliokuwa ndani ya mahakama wakati wa kusomwa kwa hukumu hiyo mji Dakar nchini Senegal, walishangilia wakati jaji alimaliza kusoma hukumu.
Bwana Habre anatuhumiwa kwa kuamrisha mauaji ya watu 40,000 wakati wa utawala wake miaka ya 80, madai ambayo ameyakana
Habre alikamatwa nchini Senegal , na kupelekwa uhamishoni mwaka 2013.

BBC
 

Gallery

Popular Posts

About Us