Ilikuwa ni ‘break up’ iliyofuatiwa na uadui mkubwa. Ilipelekea hadi Nuh Mziwanda kuandika wimbo ‘Jike Shupa’ uliomlenga ex wake Shilole.
Haikuishia hapo, wawili hao waliendelea kurushiana maneno kwenye mitandao ya kijamii na kwenye mahojiano na kulaumiana kwa mengi. Hata hivyo mlalamikaji mkubwa alikuwa Nuh aliyemwelezea Shishi kama mwanamke aliyempotezea muda wake na kumkwamisha kwenye muziki.
Pia...