KINGAZI BLOG: 05/25/16

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Wednesday, May 25, 2016

Kamati, wabunge wambana Waziri Maghembe.

Dodoma. Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii imeitaka Serikali kuteua bodi za Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa) na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Wanyamapori, ambazo zimemaliza muda. Mbali na kuteua bodi hizo, wameiomba Serikali kutoa fedha zinazotengwa kwa ajili ya wizara kwa wakati, kuiwezesha kutekeleza majukumu yake ipasavyo. Bodi ya Tanapa ilimaliza muda wake mwaka 2014. Tangu...

Mtoto wa Kabwe Agoma Kushikana Mkono na RC Makonda.

Anna Kabwe, binti wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Wilson Kabwe amegoma kumpa mkondo Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Tukio hilo la aina yake lilimfika Makonda aliposhiriki shughuli ya kuaga mwili wa Kabwe katika Viwanja vya Karimjee alipokuwa akitoa mkono wa pole kwa familia ya Kabwe. Wakati Makonda akimpa mkono, Anna aliendelea kuchezea simu yake huku akipuuza mkono...

Waziri Mkuu Akutana na Watanzania Waishio Zambia

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Watanzania waishio Zambia kwenye ubalozi wa Tanzania uliopo Lusaka Mei 24, 2016. Majaliwa alikwenda Zambia kumwakilisha  Rais John Magufuli kwenye Mkutano wa Benki ya Maendeleo ya Afrika- ADB uliofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Mlungushi. Baadhi ya Watanzania  waishio Zambia wakimsikiliza Waziri  Mkuu, Kassim Majaliwa wakatia lipozungumza...

WATU 14 WAKAMATWA MAUWAJI YA WATU WATATU MSIKITINI MWANZA

Jeshi la Polisi Nchini linawashikilia watuhumiwa 14 kufuatia tukio la mauaji ya watu watatu lililotokea katika msikiti wa Rahman eneo la Ibanda relini mkaoni Mwanza, Mei 18 mwaka huu. Akiongea na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini Kamishna Msaidizi Advera Bulimba alisema kuwa msako wa kuwakamata watuhumiwa wengine unaendelea katika maeneo mbalimbali...

Tuhuma za Kuwanyang'anya wananchi ardhi lowassa azungumza,Lukuvi naye aahidi mazito

Baada ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi kueleza Bungeni kuwa Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa alijimilikisha ardhi iliyotolewa kwa wananchi wilayani Monduli mkoani Arusha na kuahidi kuirejesha, Mwanasiasa huyo amejibu tuhuma hizo. Lowassa amesema kuwa halijui shamba alilolizungumzia Waziri huyo na kwamba hakuna ardhi ambayo anaimiliki kinyume cha taratibu. Alisema...

Mkoa wa Mwanza Unategemea Kupokea Tani 500 za Sukari

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongella, amesema mkoa wa Mwanza unategemea kupokea Tani 500 za Sukari zitakazo ingia katika mkoa huu zikitokea kiwanda cha sukari cha Kagera Sugar tarehe 24, Mei, 2016, ambazo zinaingizwa mkoani hapo na muagizaji na Msambazaji P.H  Shah. Hata hivyo mkuu wa mkoa ameonya watu watakao uza sukari hiyo kinyume na bei elekezi kuchukuliwa...

Magazeti ya Tanzania yalichoandika leo jumatano Mei 25 kwenye habari za kitaifa kimataifa na michezo

Karibu,tunakuletea kile kilichoandikwa kwenye magazeti ya tanzania leo ili ufahamu kilichojiri kwenye habari za leo.Usisahau kukaa nasi ku 'like' kwenye facebook/tanzaniampyasasa blog na twitter@tanzaniampyasasa. ...
 

Gallery

Popular Posts

About Us