KINGAZI BLOG: 05/27/16

KARIBU UHABARIKE KIGANJANI MWAKO.

Breaking News
Loading...

Friday, May 27, 2016

Juma Nkamia Adai Wapinzani Wanasura Mbaya Kiasi Kwamba Wanataka Kutapika na Wengine Meno Yao Yameoza!

Kanuni inayozuia lugha ya kuudhi bungeni ni kiinimacho kwani mbunge wa upinzani akitoa lugha inayokera, mbunge wa CCM ataomba mwongozo kwa Spika na mara akijibiwa atasimama mbunge wa CCM na kutumia lugha hiyo hiyo iliyoombewa mwongozo.

Jana Mbunge wa Chemba, Juma Nkamia (CCM) aliporomosha lugha za kuudhi baada ya kuwaambia wabunge wa upinzani waliokuwa wakishangilia kuwa wanasura mbaya hadi wanatamani kutapika.

Akichangia hotuba ya makadirio na matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa mwaka 2016/17, Nkamia alionyesha kukerwa na hotuba ya upinzani kuhusu wizara hiyo kwenye sehemu iliyozungumzia uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka jana.

Nkamia alisema uchaguzi umepita na mshindi alipatikana ambaye ni CCM na aliufananisha uchaguzi na mpira kwamba unapoisha uwanjani mtu hawezi kulalamika nje.

“Uchaguzi umeisha, leo mtu anasimama hapa anasema ‘ooh tuliibiwa kura’ mlikuwa wapi wakati mnaibiwa kura?”alihoji na kuwataka wapinzani watafute sababu kwa nini walishindwa na si vinginevyo.

"Wanajua mchezaji mmoja akiumia katika timu unachukua mwingine kwenye timu ile ile lakini inakuwaje unachukua mchezaji kutoka upinzani? Kwa hiyo niwaombe tu muwe mnatafakari kwanza,” alisema.

Hali hiyo iliibua kelele na minong’ono kutoka kwa wapinzani, jambo ambalo lilimlazimu Naibu Spika, Dk Tulia Ackson kuwataka wabunge huku akiwataja majina watulie ili mbunge huyo amalizie mchango wake.

Nkamia aliendelea, “We nyosha midomo, fanya nini lakini that is the truth (huo ndiyo ukweli). Utaongea sana na utapiga kelele sana lakini ukweli ndio huo na umekuingia vizuri.

"Mimi kelele wala hazinisumbui. Mimi nataka niwashauri kama wakati ujao mnataka kuwa chama kizuri anzeni kutafuta wachezaji wenu,” alisema.

“Nyie pigeni kelele lakini ukweli ndio huo, wenye akili wanajua na wapiga kelele wanajua na najua limewaingia vizuri sana.”

Kijembe hiki kiliwalenga Ukawa ambao katika uchaguzi mkuu uliopita walimteua aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowasa. Ukawa walimteua Lowasa baada ya kuitema na kuihama CCM ambapo alipambana na John Magufuli (CCM) aliyeshinda.

Nkamia akionekana kumlenga mbunge fulani ambaye hakumtaja jina alisema, “We piga kelele, kwanza meno yako yameoza.”

Kwa kuzingatia kanuni, lugha hiyo ni ya kuudhi lakini Dk Tulia asisitiza Nkamia amalizie kuchangia ambapo alitoa mfano wa mwandishi wa vitabu Bernard Taper aliyewahi kusema kwamba kuna watu wakiamka asubuhi wakijiangalia kwenye kioo wanatamani kutapika.

“Sasa nyie mnaoshangilia humu mna sura mbaya na mnatamani kutapika,” alisema Nkamia

Magufuli Kujaza Vijana Serikalini....Adai Wazee Ndo Wameihairibu Hii Nchi

Kuanzia sasa wateule wengi wa Rais John Magufuli serikalini watakuwa vijana kwa kuwa amegundua wengi hawapendi rushwa, amesema.

Aidha, Rais Magufuli amesema anafahamu kwamba vijana hawapendwi lakini amegundua ndio wachapakazi ambao watasaidia kulipeleka taifa katika maendeleo anayoyatamani.
  
Rais Magufuli alisema hayo jana wakati wa ufunguzi wa mkutano wa makandarasi wa mikoa ya Dar es Salaam, Mbeya na Dodoma, jijini.
  
“Nimegundua vijana wengi hawapendi rushwa, hivyo nitaongeza vijana kila nikiteua kwa kuwa niliowaweka naona matunda ya kazi zao," alisema na kuongeza kuwa: “Najua watu wanawachukia sana ila nitawaongeza.
  
“Palipo na vijana nimeona mambo yanaenda na kuna mabadiliko. Wazee ndio tumelifikisha taifa hili hapa. Hakuna asiyejua kuwa Tanzania ilichakaa kila mahala.”
  
Tangu aingie Ikulu Novemba 5, mwaka jana, Rais Magufuli amejipambanua kama mwenye kupiga vita wizi, rushwa, ufisadi, ukwepaji kodi, uzembe na ukosefu wa maadili wa watumishi wa umma.
  
Aidha, Rais Magufuli alisema idadi ya watumishi hewa imefikia 10,292 huku vijana wengi wenye ujuzi wanamaliza vyuo vikuu na kukosa ajira. Alisema kama si tatizo la uwapo wa watumishi hewa, ajira zipo kwa wingi.
  
“Nataka vijana ili twende kwa kasi, ndiyo njia pekee ya kufikia maendeleo tunayoyatarajia,” alisemna. 
  
Rais pia alizungumzia uamuzi wake wa juzi wa kuvunja Bodi ya Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) na kutengua uteuzi wa aliyekuwa mwenyekiti wake, Profesa Awadhi Mawenya.
  
Rais Magufuli alisema zaidi ya Sh. bilioni 87 zililipa mikopo hewa kwa wanafunzi 480 wenye daraja la nne kidato cha nne, huku ikiaminika mikopo ni kwa ajili ya watoto wa masikini.
  
“Unashangaa anayesimamia kitengo ni Profesa. Hapa ndiko nchi ilikofikia,”alisema.
  
Rais Magufuli alitoa mfano mwingine wa Meli kubwa 65 za makontena zilizotia nanga katika Bandari ya Dar es Salaam bila kuandikwa, ambazo alisema “hazijulikani zilielekea wapi na hazikulipwa.”
  
Baada ya Rais Magufuli kumaliza hotuba yake, alimkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda (34) kuwasalimia wajumbe wa mkutano huo.
  
Makonda alisema alipokuwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, aliunda kamati ndogo ya kufuatilia barabara na kubaini zaidi ya Sh. bilioni 2.2 zilitumika kujenga barabara ambazo mvua ikinyesha hazipitiki.
  
Alisema pia walibaini barabara zilizokuwa zikarabatiwe kwa Sh. milioni 200, zilitengewa Sh. bilioni moja kwa kila barabara na baadaye ziliombwa zaidi ya Sh. bilioni 5.9 na zilikuwa katika mchakato wa kulipwa lakini alizizuia.
  
“Manispaa ya Kinondoni ni tatizo kubwa...unakuta wananchi wanalia shida, wao wanalia kwa uongo kwa kuwa wanajua kuna fedha wanapata kama hizo.
  
“Nashukuru Mfuko wa Barabara umewanyima fedha na wameambiwa watengeneze barabara za awali hadi zikamilike kwa kutumia mapato yao ya ndani,” alisema.
  
Mbali na nafasi kadhaa za Wakuu wa Wilaya ambako habari za uhakika zinasema wengi watabadilishwa, Rais Magufuli pia ana nafasi ya uteuzi ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, baada ya kuteungua uteuzi wa Charles Kitwanga kwa sababu ya ulevi, Ijumaa iliyopita.
  
Aidha, Rais Magufuli hajateua Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga tangu atengue uteuzi wa Anne Kilango Malecela kwa kutoa taarifa ya uongo kuwa mkoa wake haukuwa na watumishi hewa Aprili, mwaka huu.
  
Rais Magufuli pia hajafikisha jumla ya Wabunge 10 anaoruhusiwa kuwateua kwa mujibu wa katiba, hivyo kuweka uwezekano wa kuwapo kwa vijana wengi zaidi serikalini kwa mara ya kwanza katika miaka 55 ya Uhuru.

Dada wa Bilionea Erasto Msuya Auawa Kinyama Kwa Kuchinjwa Nyumbani Kwake Dar es Salaam

Mtumishi wa Wizara ya Fedha, Aneth Msuya (30) ambaye ni mdogo wa Bilionea Erasto Msuya aliyeuawa kwa kupigwa risasi 22 KIA, ameuawa kwa kuchinjwa nyumbani kwake eneo la Kigamboni jijini Dar Es Salaam.

Mmoja wa ndugu wa familia hiyo, Shujaa Khamis, jana alithibitisha kuuawa kwa Aneth, lakini alikataa kuingia kwa undani.

“Ni kweli wamemchinja usiku wa kuamkia leo (jana) na hapa nipo kwenye msiba hapa nyumbani (Mererani) kwa baba. Tumeambiwa wamechukua Tv tu,” alisema.

Hata hivyo, Khamis alikataa kueleza lolote kama wana mashaka na mauaji hayo zaidi ya kuliomba Jeshi la Polisi nchini, kuchunguza kiini cha mauaji hayo na kuwasaka waliohusika.

Habari nyingine kutoka Wizara ya Fedha, ziliwakariri baadhi ya watumishi wakisema wamepata taarifa za msiba huo, lakini hawajapewa taarifa rasmi.

“Tuna taarifa tunazisikia sikia kuwa ameauawa, lakini jana (juzi) tulikuwa naye kazini ila leo (jana) ndiyo tunasikia amechinjwa na watu wasiojulikana. Imetusikitisha sana,” alisema mmoja wa watumishi hao ambaye hakutaja jina kwa kuwa si msemaji.

Kamanda wa mkoa wa Kipolisi wa Temeke, Andrew Satta alipofutwa jana kuthibitisha taarifa za mauaji hayo alisema yuko kwenye kikao.

Haya hapa Magazeti Ya Leo Ijumaa ya May 27 kwenye habari za kitaifa kimataifa,michezo.



Shule kongwe za sekondari kurudishwa kwenye ubora wake.

Serikali imeeleza mkakati wa kuzirudisha shule 33 maarufu katika ubora wake ili ziweze kufanya vizuri kama ilivyokuwa zamani.

Mkakati huo ulielezwa jana na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako alipokuwa akiwasilisha hotuba ya bajeti yake bungeni. 

Alisema shule hizo zilipokuwa nzuri zikitoa elimu bora, zilizalisha vipaji vingi, akiwamo yeye aliyesoma katika mojawapo.Alisema katika awamu ya kwanza, shule 33 zitakarabatiwa.

Alizitaja shule hizo kuwa ni Ihungo, Ilboru, Kilakala, Mwenge, Msalato, Mzumbe, Ngaza, Pugu, Same, Tabora Boys na Tabora Girls.

Nyingine ni Azania, Jangwani, Kantalamba, Mpwapwa, Tosamaganga, Malangali, Milambo, Nangwa, Kibiti, Minaki, Ifakara, Songea Boys, Ndanda, Kigoma, Kibaha na shule za ufundi za Bwiru Boys, Ifunda, Iyunga, Moshi, Mtwara, Musoma na Tanga.

 

Gallery

Popular Posts

About Us