
Katika
 ligi ya mabingwa barani ulaya Bingwa mtetezi wa ligi ya mabingwa barani
 ulaya FC BARCELONA ameungana na timu nyingine SABA kufuzu kwa hatua ya 
robo fainali ya michuano hiyo
 
Katika ligi ya mabingwa barani ulaya Bingwa mtetezi wa ligi 
ya mabingwa barani ulaya FC BARCELONA ameungana na timu nyingine SABA 
kufuzu kwa hatua ya robo fainali ya michuano hiyo baada ya kupata 
ushindi wa magoli MATATU kwa MOJA dhidi ya ARSENAL.
Mabao ya NEYMAR, LUIS SUAREZ na LIONEL MESSI yametosha kuivusha FC 
BARCELONA katika hatua ya robo fainali kwa ushindi wa jumla ya magoli 
MATANO kwa MOJA dhidi ya ARSENAL.
 Bao pekee la kufuta machozi kwa ARSENAL katika mchezo wa jana 
uliofanyika nyumbani kwa FC BARCELONA, CAMP NOU limefungwa na kiungo 
MOHAMED ELNENY.