Rais
 JOHN MAGUFULI amewataka watanzania kufanya  kazi kwa bidii ili 
kuharakisha maendeleo ya nchi na kukuza uchumi wa taifa ikiwa ni sehemu 
ya kuondokana na umasikini nchini
Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli  
akisalimia waumini huku akisikilizwa na Askofu Mkuu wa Dayosisi ya 
Mashariki na Pwani  Kanisa la Kiinjili la Kilutheri
Tanzania Dkt. Alex Malasusa na Mchungaji Chalres Mzinga baada ya Ibada ya Pasaka katika Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam leo Machi 27, 2016
Rais MAGUFULI amesema hayo Jijini DSM katika  Ibada ya 
PASAKA alipopata fursa  ya kuwasalimu waumini  wa Kanisa la Kiinjili la 
Kirutheri AZANIA FRONT alipokwenda kusali pamoja na mkewe mama JANET 
MAGUFULI.Tanzania Dkt. Alex Malasusa na Mchungaji Chalres Mzinga baada ya Ibada ya Pasaka katika Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam leo Machi 27, 2016
Pamoja na mambo mengine Rais MAGUFULI amesema kipindi hiki cha sikukuu watanzania wanapaswa kudumisha upendo na kujenga umoja kwa taifa zima ili kufikia malengo mbalimbali ya maendeleo.
Awali akitoa mahubiri katika ibada ya pasaka Askofu wa Kanisa la Kiinjili la kiluteri Tanzania Dayosisi ya Mashariki na Pwani Dokta ALEX MALASUSA alisema wananchi wote wanapaswa kuwa na hofu ya Mungu ili kuweza kushinda changamoto mbalimbali katika jamii ikiwemo rushwa.